Alhamisi, 23 Mei 2019

Mobile Saloon za Kiume

MOBILE BARBER SHOP
Nimetumia jina maarufu, lakini najua wengi mnafahamu kuwa namaanisha saluni ya kiume. Biashara ya saluni ya kiume ni kubwa na imepanuka. Ni biashara ya uhakika kwa sababu kati ya mambo muhimu mjini watu wanayozingatia ni usmart.
Kama wewe ni kinyozi hili ni dili zuri kwako. Siyo kila mtu ana muda. Wengine wana fedha lakini hawana muda. Kuna watu wanapenda kunyoa nywele, ndevu na huduma nyingine za saluni kama kufanya steaming, waves, black, facial, scub nk kila wiki lakini hawana muda wa kwenda saluni.
Changamkia hii dili. Kazi yako ni kununua mashine zako mbili na vifaa vingine vya kawaida, kisha unapachika jina mathalani JULIUS MOBILE BARBER SHOP. Utapiga pesa nzuri sana.
Kumbuka kwa sababu ni huduma ya kumfuata mtu kwake, bei haitakuwa ileile. Kwa wastani (kwa aina ya watu ninaowazungumzia hapa) bei ya kunyoa saluni ni wastani wa Tsh. 5000 (nywele na ndevu) kwa saluni nyingi za mijini.
Hapo bado scub, waves na huduma nyingine kama atapenda ambazo kwa watani mteja mmoja hugharamia si chini ya Tsh. 10,000. Ukimfuata kwake, itakuwa mara mbili au tatu na pengine ukalipwa zaidi kulingana na utakavyotoa huduma.
Kuna wagonjwa, wazee na watoto ambao ndugu zao hawataki usumbufu wa kuwapeleka saluni. Kuwa mjanja kwa kuchungulia hii fursa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni