Alhamisi, 23 Mei 2019

Ufugaji wa Nguruwe

ELIMU YA UJASILIAMALI JUU YA UFUGAJI WA NGURUWE

MCHANGANUO MDOGO WA MRADI WA NGURUWE
-Nguruwe watoto 20 @ 20,000 = 400,000
– Banda la mabanzi=1,000,000
– Chakula = 1,000,000
– Dawa= 200,000
After 1yr: Nguruwe 20 watazaa vitoto kama 160,utachakuwa vitoto jike 100,
mama zao wote watauzwa, huku shambani kwetu nguruwe
mkubwa ni Tsh 200,000 tu, utapata 4,000,000.
After 2yrs: Nguruwe 100 wanaweza kuzaa 700. Kati ya 700 chagua majike 500,(unaweza kuuza watoto dume ukanunua jike).
Year 3: Nguruwe 500 watazaa watoto 3500, chagua watoto 1500 tu
Kutoka hapo unamentein Number 1500, kila mwaka unaweza kuuza
watoto zaidi ya 3000, na nguruwe wakubwa 1500.
1500*200000= Tsh 300,000,000/= kwa mwaka
Nusu ya hiyo pesa ni gharama zingine, unabaki na 150mil.
Kabla hujajitumbukiza kaone mifano, au nenda chuo cha sokoine (SUA) na vyuo vingine vya kilimo na mifugo ukaonane na wataalamu au tembelea maofisa ugani na wataalam mbalimbali wa mifugo au wafugaji wenye uzoefu.
ZIJUE KANUNI KUU NNE KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE.
Je unazifahamu aina za nguruwe na sifa zake,
Zifuatazo ni aina za nguruwe zinazo fungwa kwa wingi  nchini Tanzania ambazo pia mfugaji yeyote anaweza kufuga kwani upatikanaji wake ni rahisi kwa maeneo yaliyo mengi.
Large white.
Nguruwe hawa wana rangi nyeupe mwili mzima
Masikio yao yanakuwa yamesimama mda wote.
Nyuso zao zimeingia kwa ndani kidogo (muonekano wake upo kama dish)
Saddleback
Wakubwa tofauti na aina nyingine za nguruwe.
Masikio yamelala kiasi
Landrace
Wana ukubwa wa wastani
Wana rangi nyeusi na mstari mweupe kuzunguka shingo na miguu ya mbele.
Mara baada ya kuzijua aina za nguruwe na sifa zake, sasa zijue kanuni za msingi katkia ufugaji wa nguruwe.
Mambo ya msingi kwa ufugaji wa nguruwe.
– Chagua koo zinazo zalisha vyema.
Uchaguzi wa koo huchangia zaidi ya asilimia 80 katika mafanikio ya ufugaji wa nguruwe, chagua koo amabayo ina  zalisha watoto wengi na wenye afya.
Kwa mfugaji ambaye anataraji kununua nguruwe kutoka kwa mfugaji mwingine, Zingatia sana kumbukumbu zilizo wekwa na mfugaji yule na cha msingi ziwe sahihi hii itakupa picha ya kujua uzazi wa nguruwe huyo.
– Jenga banda bora.
Jenga banda ambalo linaendana na idadi na ukubwa wa nguruwe, banda ambalo halitapitisha mwanga mkali wa jua, upepo mkali,pia litakalo himimili mikimiki ya nguruwe wakorofi, hii itasaidia kupunguza usumbufu na bugudha kwa nguruwe na hatazalisha bila shida kwa nguruwe anayeishi katika nyumba yenye bugudha na usumbufu uzalishaji wake upungua sana uzalushaji.
– Zingatia afya bora kwa nguruwe.
Sote tunafahamu afya ni kitu cha msingi sana iwe kwa binadamu na hata mnyama hivyo, Afya bora ya nguruwe ni kitu cha msingi sana kuzingatiwa kwa kwa nguruwe asiye na afya bora udhoofika na uzalishaji wake hushuka kwa kiwango kikubwa sana..
Afya bora hutokana na kufanya, Chanjo dhidi ya magonjwa kama minyoo.
– Walishe wanyama chakula bora.
Chakula cha nguruwe ni muhimu kiandaliwe kulingana ma umri wa
nguruwe na mahitaji katika mwili wa nguruwe
Chakula cha nguruwe kiwe katika uwiano sahihi hii, chakula ambacho kita kidhi mahitaji ya mwili na uzakushaji kuwa mkubwa.
Nguruwe hapatiwe chakula chenye vyanzo vya madini, vitamin na protini.
Vyakula venye vyanzo vya protini husaidia sana katika kujenga mwili.
Vitamin na madini vyakula venye vyanzo hivi vinahitajika kwa wigni hasa calcium na phosphorus kwa nguruwe wa kunenepesha na walioachishwa kunnyonya.
Epuka kuwapa nguruwe kuwapa chakula chenye chumvi nyingi kwani hii itamfanya nguruwe kunywa maji mengi sana na matokeo yake nguruwe huarisha sana natimaye ukuaji wake huwa wa polepole. Hata hivyo kumbuka chumvi uongeza radha ya chakula na uwekaji wake katika mchanganyo wa chakula uwe ni asilimia 0.5 tu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni